Friday, November 19, 2010

Mhe.Mrema, unatuma sms au …!

BADO NAKUPENDA USIJALI KIONGOZI

Dodoma
Bunge la 2010-2015 ni la vijana, mandhari na kila kitu kinabeba tafsiri hiyo na hapa kuna ripoti kamili ya kilichochukua nafasi mjini Dodoma wakati wa ufunguzi wa Bunge la 10.
Bunge.
Jicho la Ijumaa Wikienda bungeni lina tathmini ya jumla kuwa bunge jipya lina idadi kubwa ya vijana kuliko wazee, tofauti na ilivyozoeleka miaka ya nyuma.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndicho pekee kinachoongoza kwa kutumbukiza wazee mjengoni, ingawa vijana ni wengi zaidi, kikifuatiwa na Chama cha Wananchi (CUF).
John Mnyika, Ubungo.
Chama cha NCCR-Mageuzi, ndicho kilichotia fora zaidi kwa kuingiza wabunge wanne na kati yao robo tatu ni vijana chini ya umri wa miaka 30, isipokuwa mwana mama Agripina Zaitun Buyogera wa Kasulu Vijijini.

NCCR kimevunja rekodi ya CHADEMA katika bunge lililopita, wakati mbunge wake, Zitto Zuberi Kabwe alipoingia mjengoni akiwa na umri wa miaka 28, hivyo kuwa kijana mdogo zaidi kutoka jimboni.
Mchungaji Peter Msigwa, Iringa Mjini.
Safari hii, Mbunge wa Muhambwe, Felix Mkosamali (NCCR) ndiye mbunge mdogo zaidi ambapo ameingia mjengoni akiwa na umri wa miaka 24.

JUMANNE, MPAKA ALHAMISI ILIYOPITA
Idadi ya wabunge waliowasili kwa ajili ya kujisajili ilikuwa ndogo Jumanne, siku iliyofuata (Jumatano) iliongezeka lakini walifurika Alhamisi ambapo ndiyo ilikuwa mwanzo wa utambulisho bungeni.
Catherine Magige, Viti Maalum (UVCCM- Arusha) .
Mandhari ya Jumatano yalikuwa ni yenye kuchangamka, wabunge wakipongezana kwa kufanikiwa kushinda, wengine wakirejea na wale waliofanikiwa kwa mara ya kwanza.

SLAA, MBOWE WAITEKA DOM USIKU
Msafara mkubwa wa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Willibrod Slaa na mwenyekiti wake, Freeman Mbowe uliwasili Jumanne usiku mjini Dom na kufanya mkutano kwenye makao makuu ya chama mkoa.
David Kafulila, Kigoma Kusini.
Mkutano ulipambwa na shamrashamra, wakazi wa Dom wakimshangilia Slaa alipokuwa anawasili na hata alipoanza kuhutubia.

Hata hivyo, baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Osmund Mbilinyi ‘Sugu’ kuwasili kwenye mkutano huo, wananchi walipoteza umakini kwa Slaa na kuanza kumshangilia shujaa huyo wa Bongo Flava.
Zitto Kabwe, Kigoma Kaskazini.
Busara za Slaa, zilimuongoza kumwita mbele Sugu a.k.a Mr. II aweze kuwasalimia wananchi kwa uwazi na baada ya hapo mkutano ulifungwa.

SITTA AVUTA HISIA
Jumatano majira ya saa 5 asubuhi, Spika wa Tatu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samuel Sitta aliwasili bungeni kujisajili na kuzungukwa na umati mkubwa wa watu, wengi wakiwa ni waandishi wa habari na wabunge.
Ezekia Wenje, Nyamagana.
Akiwa mwenye uchangamfu, alikuwa akiwatania wabunge hasa wale waliopita mbali naye, huku akiwakumbusha kwamba yeye ni mgombea wa uspika.

HARUFU MBAYA BUNGENI
Dalili ya hatari ndani ya CCM na bunge, zilionekana kwenye viunga vya bunge kutokana na kampeni za waziwazi ambazo zilikuwa zinaendeshwa.
Lucy Mayenga, Viti Maalum (Wanawake-Shinyanga).
Makundi ya wazi yalionekana, upande mmoja ukitaka Sitta apite, wakati mwingine ukishinikiza aenguliwe mapema.

Upande mmoja ulikuwa ukiwaomba wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM (CC), wakate jina la Sitta kwa kile walichodai kwamba matokeo ya kushuka ilichopata chama hicho katika Uchaguzi Mkuu uliopita yalisababishwa na yeye.
Halima Mdee, Kawe.
Hata hivyo, upande wa pili, walidai Sitta ndiyo sababu ya ushindi wa CCM katika Uchaguzi Mkuu 2010, vinginevyo chama hicho kingeangushwa mwereka mkubwa.

Walidai kuwa uongozi wa Sitta ulionesha wananchi kwamba ndani ya CCM kuna watu makini walio tayari kujikosoa ndiyo maana wakakipigia kura.
Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu, Mbeya Mjini.
KIGOGO AVUJISHA SIRI YA KAMATI
Jumatano, saa saba mchana, kigogo mmoja wa chama alivujisha siri alipowasili bungeni baada ya kumnong’oneza mbunge mmoja kwamba mwaka huu spika atakuwa mwanamke.

Sababu alizotoa, ndizo zilizoonekana katika taarifa rasmi kwa vyombo vya habari, iliyosainiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, John Chiligati siku hiyo hiyo jioni.
WAHESHIMIWA CLUB 84
Jicho la Ijumaa Wikienda lilizama ndani ya Club 84 ambayo ina jina kubwa na kujionea waheshimiwa kadhaa (majina tunayo) wakijirusha, huku wengine wakiondoka eneo hilo karibu na majogoo.

BUNGENI KIMYA
Alhamisi kwa watu wengi ilikuwa kama msiba bungeni, wakisikitikia uamuzi wa kamati, ikiwemo wafanyakazi wa bunge lakini hakukuwa na jinsi.
Kikao cha kamati ya Wabunge wa CCM, kilikaa kuchagua kati ya majina matatu, Anna Makinda, Anna Abdallah na Kate Kamba ambapo jina la Makinda liliposhinda, shamrashamra zilianza.

Wakati hali ikiwa hivyo, CHADEMA kilikuwa ‘bize’ na vikao, kuunda Kambi ya Upinzani Bungeni.
Idd Azzan, Kinondoni.
DOM GESTI, HOTELI
Tathmini Dodoma, kila mtaa kuna gesti na hoteli kadhaa na kwa hesabu, bila shaka ndiyo mkoa wenye gesti na hoteli nyingi Tanzania.

MADENTI U-DOM
Wanafunzi wanaosoma Chuo Kikuu cha Dodoma (U-Dom), walionekana wakirandaranda kwenye hoteli za waheshimiwa, na walipatikana pia mitaani wakati huu wa bunge jipya.
Neema Mgaya Hamid (Viti Maalum, UVCCM-Dar)
NI MREMBO?
Bunge lililopita lilikuwa na warembo wengi lakini mwaka huu ni ‘funika bovu’.

Nani mkali ni mchuano kati ya Mbunge wa Viti Maalum (UVCCM), Catherine Magige ‘Pamela’, Mbunge Viti Maalum CCM (Geita), Vicky Kamata ‘Madame V’ na Mbunge wa Kawe (CHADEMA), Halima Mdee.
Vita Kawawa,
Wengine ni Mbunge wa Viti Maalum CCM (Shinyanga), Lucy Mayenga, Mbunge wa Viti Maalum CHADEMA (Kigoma), Mhonga Ruhanywa, Mbunge wa Viti Maalum (UVCCM), Neema Mgaya Hamid na Mbunge wa Viti Maalum CCM (Zanzibar), Tawhida Cassian Gallus.

HANDSOME BOYS
Ingizo jipya la wabunge vijana linafanya mchuano uwe mkali katika bunge hili.
Mnyika na David Silinde wakibadilishana mawazo.
Zitto, Mkosamali, Sugu wamo kwenye orodha, halafu wapo wengine kama Mbunge wa Ubungo (CHADEMA), John Mnyika, Mbunge wa Bumbuli (CCM), January Makamba na Mbunge wa Mbozi Magharibi (CHADEMA), David Silinde.

Wengine ni Mbunge wa Nyamagana (CHADEMA), Ezekia Wenje, Mbunge wa Ilemela (CHADEMA), Highness Kiwia, Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA), Godbless Lema na wengineo.
Sugu na Mnyika wakipata msosi.

Thursday, November 18, 2010

AHAMED KHALFAN GHAILANI, MTANZANIA MWENYE KESI YA MAUWAJI.

Mshukiwa wa ugaidi, Ahmed Khalfan Ghailani ametajwa jana na mwendesha mashtaka katika mahakama ya Manhattan nchini Marekani kama ‘muuaji wa halaiki’.

Ghailani anatuhumiwa kuhusika katika miripuko ya mabomu mwaka wa 1998 katika balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania.

Katika mchango wake wa mwisho katika kesi hiyo, mwendesha mashtaka wa mahakama ya Manhattan, Harry Chertoff alisema Bw Ahmed Khalfan Ghailani ambaye alikuwa ameketi viti kadhaa upande wake wa kushoto, ni muuaji wa halaiki ambaye ana alama ya damu ya mamia ya watu mikononi mwake.

Ghailani, Mtanzania anayetokea Zanzibar, ana umri wa miaka 36 na anahusishwa pakubwa na kupanga miripuko ya mabomu katika balozi za Marekani mjini Nairobi na Dar es Salaam mwaka wa 1998 iliyosababisha vifo vya zaidi ya watu 200.

Mshukiwa huyo alikana makosa hayo na anahusishwa pakubwa na mtandao wa Al-Qaeda katika kanda ya Afrika mashariki.

Kesi yake ni ya kwanza ya washukiwa waliokuwa wameshikiliwa katika gereza la Guantanamo nchini Cuba, kusikilizwa katika mahakama ya kiraia.

Mahakama ya Manhattan ni hatua chache kutoka katika jengo la mnara wa World trade centre ambapo shambulio la kigaidi la Septemba 11 mwaka 2001, lilitekelezwa na wanachama wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda.

Wachunguzi wanalinganisha uhusiano huo kama hatua kubwa ya kutanzua kitendawili cha mashambulizi ya kigaidi.

Rais Barack Obama wa Marekani alitoa amri ya kufungwa kwa mahakama ya kijeshi ya Guantanamo na washukiwa wanaoshikiliwa wafunguliwe mashtaka katika mahakama ya kiraia.

Azimio hilo lilipingwa vikali na wachunguzi kadhaa wakidai kwamba uzito wa kesi hizo za ugaidi haufai kushughulikiwa katika mahakama za kiraia.

Jaji, Lewis Kaplan amesema kesi hiyo inaweza kuendelea hadi mwakani.

Khalfan Ghailani alikamatwa mwaka wa 2004 akiwa nchini Pakistan.

Dk Willbrod Slaa]

Viongozi wa dini wamtuliza Dk Slaa Send to a friend
Monday, 08 November 2010 01:07
0diggsdigg
[Dk Willbrod Slaa] Salim Said
JOPO la viongozi wa dini limefanya ziara ya ghafla kwa aliyekuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Wiilibrod Slaa na kumtaka akubali matokeo au atumie njia za kisheria kudai haki yake, Mwananchi imebaini.

Dk Slaa hakutokea kwenye hafla ya kutangaza mshindi wa kiti cha urais wala sherehe za kuapishwa kwa Jakaya Kikwete kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano na aliahidi kuwa angetoa tamko zito jana.

Wakati Tume ya Uchaguzi (Nec) ikiendelea kutangaza matokeo, Dk Slaa aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kueleza kuwa hangekubaliana na matokeo kutokana na kubaini kuwa Nec ilikuwa inatangaza matokeo tofauti na yaliyo kwenye nyaraka walizosaini na hivyo kuitaka isitishe zoezi hilo ili kura zianza kuhesabiwa upya.

Dk Slaa pia aliituhumu Idara ya Usalama wa Taifa kuwa ilihusika kuchakachua kura kwa lengo la kumbeba mgombea mmoja wa urais, tuhuma ambazo ziliifanya taasisi hiyo, inayofanya kazi kwa siri, ijitokeze hadharani kujibu na kumuelezea katibu huyo mkuu wa Chadema kuwa "ni mzushi".

Tamko hilo la Dk Slaa lilionekana kuwashutua viongozi wa dini na kuhisi dalili za kutokea mvutano ambao ungeweza kusababisha kuvunjika kwa amani. Mwananchi imebaini kuwa ziara ya kimya kimya ya viongozi hao wa dini ilifanywa wiki iliyopita kabla ya Nec kumtangaza Kikwete kuwa ni mshindi.

Kwa mujibu wa habari zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kwamba viongozi hao walimtaka Dk Slaa asisababisha mvutano ili kudumisha amani ya nchi. Habari za ziara hiyo ya dharura ya jopo hilo la viongozi wa dini za Kikristo na Kiislamu zilithibitishwa na meneja wa kampeni wa Chadema, Profesa Mwesiga Baregu. Profesa Baregu aliiambia Mwananchi kuwa ujumbe mkubwa uliofikishwa na jopo hilo ulikuwa ni kuwaomba viongozi wa Chadema kutumia njia sahihi za kudai haki yao ambazo hazitazusha vurugu, fujo wala uvunjifu wowote wa amani.

“Ujumbe wao kwetu ulikuwa ni kutuomba kwamba kusiwe na vurugu, fujo wala uvunjifu wowote wa amani wakati wa kutangazwa matokeo na hata baada ya kutangazwa,” alisema Profesa Baregu. “Badala yake wakatuomba kama hatujaridhika na matokeo basi tutumie taratibu za kisheria zilizowekwa kudai haki. Lakini sisi tuliwaeleza kuwa hatuna nia ya kufanya vurugu wala kuandamana, lakini uchaguzi umevurugwa na hatuwezi kukubali.”

Alisema jopo la viongozi hao wanne wa dini wakiongozwa na askofu mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dk Valentino Mokiwa lilifanya ziara hiyo baada ya Chadema kuitaka Nec kusitisha utangazaji wa matokeo kwa kuwa Usalama wa Taifa wamechakachua matokeo.

“Sijui walikuwa na wasiwasi gani au nani aliwashauri kuja tena kuonana na viongozi wa Chadema, lakini nadhani ni baada ya kuona tumesema hatungekubali matokeo kwa kuwa uchaguzi umechafuliwa,” alisema Profesa Baregu. Alisema pamoja na wasiwasi huo wa viongozi wa dini, Chadema haikuwa na mpango wowote wa kuunganisha nguvu ya umma na kuingia barabarani, kama ilivyofanyika Kenya, kudai haki. “Lakini hatujaridhika na matokeo kwa sababu uchaguzi ulikuwa mchafu.

Rais amechaguliwa na robo tu ya wapigakura. Nec imeongeza majina kwa sababu kabla ya uchaguzi ilisema wapigakura wote ni 19.9 milioni, lakini akitangaza mshindi Jaji Lewis Makame anasema ni 20.1, hatujui wametoka wapi,” alisema Profesa Baregu. Kwa mujibu wa Baregu wengine waliokuwamo katika msafara huo wa viongozi wa dini walikuwa ni kutoka Kanisa Katoliki na Baraza Kuu la Waislaam Tanzania (Bakwata).

Dk Slaa, ambaye alishika nafasi ya pili kwenye kinyang'anyiro cha urais kwa kupata asilimia 26 ya kura, pia alitembelewa na jopo la viongozi wa dini kabla ya kumalizika kwa kampeni wakimtaka awe tayari kupokea matokeo yoyote yale. Jopo hilo lilidai wakati huo kuwa lingetembelea wagombea wengine wa urais, lakini halikufanya tena ziara kwa wagombea wengine hadi uchaguzi ulipofanyika.
HARAKATI za serikali kuboresha huduma za afya, zimepata msukumo mpya baada ya Shirika la Pharm Acces la Uholanzi, kutenga zaidi ya Euro 2 milioni sawa na Sh400 bilioni kuboresha hospitali na zahanati binafsi nchini.
Pia, Pharm Acces limeanzisha mpango wa bima ya afya kwa watu walio katika sekta isiyo rasmi, tayari limeanza kutoa huduma hizo Dar es Salaam na Arusha kwa kushirikiana na Chama cha Watoa Huduma za Afya nchini (APHFTA).

Wakizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mipango wa Pharm Acces, Geert Haverkamp na Meneja Mipango wa APHFTA, Dk Samwel Ogillo, walisema chini ya mpango wa utoaji mikopo, wamiliki wa hospitali binafsi watapatiwa mikopo nafuu.

Haverkamp alisema Tanzania ina changamoto kubwa katika bajeti ya afya na upatikanaji fedha, huku akionyesha tofauti na nchi za Ulaya na Marekani, mtu mmoja hutengewa Sh1 milioni kwa afya kila mwaka, Tanzania hutengewa Sh22,000.

Kutokana na hali hiyo, alisema Pharm Acces imejipanga kuwezesha watoa huduma za afya kupitia sekta binafsi ili kuboresha nyenzo na huduma wanazotoa kwa wananchi.
Kwa kuzingatia hali hiyo, Pharm Acces imetenga Euro 2 milioni kusaidia kuboresha huduma za afya kupitia sekta binafsi.

Naye Dk Ogillo alifafanua kuwa uwezeshaji huo, utakwenda sanjari na utoaji mafunzo ya biashara kwa wamiliki wa zahanati, na hospitali binafsi.
Alisema vigezo vitakavyowezesha wamiliki na watoa huduma za afya kupata mikopo ni uanachama wa APHFTA na yule anayetunza vitabu vya hesabu za zahanati, kilinini au hospitali yake.

About Professor Wangari Maathai

About Professor Wangari Maathai

Professor Wangari Muta Maathai was born in Nyeri, Kenya (Africa) in 1940. The first woman in East and Central Africa to earn a doctorate degree, Professor Maathai obtained a degree in Biological Sciences from Mount St. Scholastica College in Atchison, Kansas (1964). She subsequently earned a Master of Science degree from the University of Pittsburgh (1966). Professor Maathai pursued doctoral studies in Germany and the University of Nairobi, obtaining a Ph.D. (1971) from the University of Nairobi where she also taught veterinary anatomy. She became chair of the Department of Veterinary Anatomy and an associate professor in 1976 and 1977 respectively. In both cases, she was the first woman to attain those positions in the region.

Professor Maathai was active in the National Council of Women of Kenya in 1976-87 and was its chairman from 1981-87. In 1976, while she was serving the National Council of Women, Professor Maathai introduced the idea of community-based tree planting. She continued to develop this idea into a broad-based grassroots organization whose main focus is poverty reduction and environmental conservation through tree planting. With the organization which became known as the Green Belt Movement Professor Maathai has assisted women in planting more than 40 million trees on community lands including farms, schools and church compounds.

Wednesday, November 17, 2010

ARUSHA

TO DAY IS WEDNESDAY 17TH NOV 2010. AM STILL IN ARUSHA REGION SINCE MONDAY 15TH NOV TO ATTEND A WORKSHOP OF THE USE OF INTERNET FOR JOURNALIST.TO DAY OUR TRAINING CONSULTANT WHICH ALSO IS OUR TEACHER,MR.PEIK JOHANSSON TEACH US ABOUT WEBSITE AND AM VERY PROUD OF THAT, I LEARN MUCH ABOUT WEBSITES. EXAMPLE, AJOL WEBSITE, AFRICA WEBSITE, ALSO HOW TO FIND OUT THE PRESDENT OF ANY COUNTRY, THE PRIME MINSTERS, THE CAPITAL CITY OF COUNTRY AND HISTORICAL BACKGROUND.

Tuesday, November 16, 2010

Leo nimesoma jambo jipya sana katika mafunzo hasa jinsi ya kuandaa bloge

Monday, November 15, 2010

susan profile

SUSAN PROFILE.

MY NAME IS SUSAN NGEIYAMU, A RADIO JOURNALIST AND PRESENTER. FOR THE TIME BEEN AM WORKING WITH RADIO VOICE OF THE GOSPEL MOSHI KILIMANJARO EAST AFRIKA. AM A MOTHER OF TWO SONS, JOEL AND JOHNSON. BY THE TIME BEEN AM ATTENDING A WORK SHOP ABOUT INTERNET USE FOR JOURNALIST, ORGANISED BY MISA TAN TANZANIA THE WORK SHOP TAKING PLACE AT UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM COMPUTING CENTRE ARUSHA BRANCH. IT IS MY WISH THAT AFTER 5 DAYS OF WORK SHOP AM GOING TO ACHIVE SOME THING GOOD FOR MY LIFE.